Sanaa kioo cha jamii


Msanii Afande Sele alipataga kutunga wimbo uliotwa, “darubini kali”, ambao ulimwongezea umaarufu hadi kumsaidia kushinda tuzo ya Mfalme wa Rhymes. Nyimbo ya “darubini kali”, ilizungumzia mambo mbalimbali ya jamii. Nyimbo hiyo pia ilifanikiwa kuonyesha uhusiano kati ya kazi ya sanaa, mfano sasa Bongo Flava, na jamii inayozungukwa nayo. Katika maneno yake mwenye, Afande alisema, “mimi ni msanii, mimi ni kioo cha jamii”, hivyo kujenga hoja kuwa sanaa ni chombo ambacho kinatumia fasihi kuyaweka bayana matatizo yaliyomo ndani ya jamii zetu.

Hivyo basi, leo hii ninadiriki kusema bongo flava inakibarua kikubwa cha kuzungumzia maswala ya jamii ya sisi vijana. Sanaa hii inatoa moja kati ya nafasi chache ambazo vijana tunazo kuelezea na kujadili matatizo yetu. Pamoja na ukweli kuwa zipo nyimbo ambazo zinazungumzia matatizo haya, lakini ubunifu wa kisanii si wakuridhisha sana. Mimi ninaamini, ili sauti ya msanii iweze kusikika na watu wengi, lazima kazi ya msanii iwe na ubunifu utakaofanikisha kutofautisha kazi yake na kazi za wasanii wengine. Sasa basi, kwakuwa swala ni kuwakilisha vijana na kuwasilisha matatizo ya vijana, nimefurahishwa sana na nyimbo hii ya “samahani wanangu” ya msanii Mrisho Mpoto. Bwana Mpoto amezungumzia matatizo yetu vijana na baadhi ya vyanzo vya matatizo hayo.

Nitapenda sote tusikilize maudhui yaliyomo ndani ya kazi hii ya kisanaa na kuwa makini katika kusikiliza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika nyimbo hii.

Mrisho Mpoto na ‘Samahani Wanangu”

Mrisho Mpoto akihojiwa na starlink

Previous ArticleNext Article
Bahati was born and raised in Tanzania, and then moved to California to pursue his college education. He graduated in 2008 with a Bachelor’s Degree in Political Science and a minor in Sociology. Bahati expects to be doing his Masters in African Studies in the near future. He is currently working on starting a t-shirt business and a possible publication of some of his writings. One thing that Bahati cannot live without is music, specifically Hip Hop & Bongoflava which he argues are both the voice of the youth today, and is excited to look into how Bongoflava can be a source of further entrepreneurship among the youth in Tanzania. Bahati believes that Bongoflava can help to reduce poverty in Tanzania, as can a more collective effort among key players.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend