Wageni karibuni!

Kutokana na juhudi za wenzetu, nadhani leo idadi ya watembeleaji kutoka Dar es Salaam (hasa UDSM) imeongezeka zaidi ya maradufu!

Kwahiyo, napenda kuchukukua fursa hii kuwakaribisha (wageni na wenyeji): Karibuni kwenye tovuti yenu ya Vijana FM!

Ukiacha filamu fupi zinazotoa mafunzo mbalimbali kupitia hadithi na mahojiano (ya kitaaluma, burudani, shughuli za kijamii n.k.), kuna kurasa ambazo itakuwa jambo la busara mkiperuzi; ukiona kitu ambacho kitamfaa mwenzako, usikalie taarifa, bali jaribu kumtumia.

Kuna kurasa zifuatazo:

Pia, tumepata kuwa na makala zilizozua mijadala mizuri:

Mijadala niliyoitaja hapo juu inaweza ikafufuliwa (kwa kuisogeza mbele) kama tukiona watu wanaendelea kutoa maoni!

Msisite kuwasiliana nasi au kutuma makala — tuna timu ya wahariri wa Kiswahili na Kiingereza (samahani sana kwa wale wanaopenda kujadili mambo kwa Kichagga, Kipare, Kihaya, Kisukuma…). Pia, unaweza kututumia maoni kupendekeza vitu gani kwenye tovuti viboreshwe.

Shukrani.

Previous ArticleNext Article
Steven was born and raised in Dar es Salaam, and moved to Germany for his studies. He graduated with a BSc. in Physics (Jacobs University Bremen), and then a MSc. in Engineering Physics (Technische Universität München). Steven is currently pursuing a PhD in Physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the Netherlands. He’s thinking about starting his own business in a few years; something high-tech related. At Vijana FM, Steven discusses issues critical to youths in Tanzania, music, sport and a host of other angles. He’s also helping Vijana FM with a Swahili translation project.

This post has 4 Comments

4
  1. Shukrani Jack D kwa kuja hapa mara kwa mara! Tunajua tukiweka makala hapa, watu wafuatao lazima wataipitia (na mara nyingi wataacha maoni): Jack D, Nionavyo, Subi, Vin, SL, Mzee wa Changamoto, Bata, Bihemo, Dr. Mallaba… orodha ni ndefu, lakini hayo majina ninayaona mara nyingi.

    Pia itakuwa si busara kutowashukuru wale waliokubali “kuhojiwa”; na kubadilishana taarifa na ujuzi (kwenye masuala ya kutafuta vyuo, taaluma n.k.).

  2. Nafurai sana kwa wale wa2 mnao22mia hizi ambazo zip juu ya ku2elimisha vijana na ku2fanya 2fikilie mbali kupitia maisha yetu yapoje au yatakuwaje huko mbele (this time 2morro ) kwa kweli natoa pongezi zangu za dhati kwa wale wote mnao tuamsha kw.mf. ile ishu iliyopita ya jitambue kipaji chako nikweli jama 2jalibu ku2mia muda mwingi kwa kufikiri kubuni na sio kwa kufikiri eti unakaa na wenzako mnadai eti Diamond sijui atatoalini wimbo mpya jiangalie nawewe pia .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend