Nasaha za Hayati Salim Ali Kibao juu ya Kiswahili

Je wafahamu maneno asilia ya Kiswahili ambayo ni mbadala ya haya: damu, maiti, harusi, karibu, tafadhali? Ukiombwa utaje neno la Kiswahili lenye kumaanisha vinyweleo vilivyomo chini ya midomo ya wanaume, utasema nini? Matumizi yapi ya maneno ya Kiswahili ni sahihi? Fazaa au fadhaha? Huzuni au hudhuni?

Haya ni machache tu ambayo msomi wa lugha ya Kiswahili, hayati Salim Ali Kibao, aliyaeleza katika maongezi yake na wanahistoria yaliyorekodiwa mwaka 1995. Chondechonde msikilize.

Kila wakati huwa ninastaajabu nikisikiliza mawaidha kama haya. Mara nyingi yananifanya nisite kujieleza kwa wengine kuwa Kiswahili ni lugha yangu mama. Cha kusikitisha ni kwamba lugha hii inazidi kutenguliwa kadiri miaka inavyoenda. Katika uwanja na wakati huu tunalilia Kiswahili, ingali tunafahamu kuwa lugha kadhaa za kikabila katika ukanda huu wa Afrika nazo zinazidi kufa kila dakika. Lugha ndogo zinakufa kwasababu ya Kiswahili. Kiswahili halisi nacho kinakufa kwasababu ya matumizi mapya ya kurahisisha semi (pindi lugha inaposambaa, ikijumuishwa ukuaji wa matumizi ya Kiingereza na lugha ngeni nyingine). Mwisho wa siku mzungumzaji anayechimbuka katika maeneo haya angali mtu mzima atafahamu salamu za lugha ya kabila tu, ataongea Kiswahili hafifu (Swanglish), na kwenye Kiingereza matumizi yake nayo yatakuwa duni. Majanga matatu kwa mpigo! Jiulize, kizazi kitakachomfuata kitatumia lugha ipi?

Makala na kurasa nyingine:

Previous ArticleNext Article
Joji was born and grew up in Dar es Salaam, Tanzania. He graduated with a B.Sc in Biochemistry in Germany, and is now pursuing a Masters degree in Microbiology & Immunology at the Swiss Federal Institute of Technology (ETH) in Zurich, Switzerland . Joji is particularly interested in matters related to global health, and basic science research that tackles public health challenges. He is engaged in mentoring Tanzanian students in higher education issues, most notably at the Kibaha High School. In this capacity, Joji blogs with Vijana FM about scientific research and development, and how youth can gain greater access to higher learning.

This post has 2 Comments

2
  1. Ningependa kukipendekeza kipindi cha ‘Ulimwengu wa Kiswahili’ kinachorushwa na TBC1 kila Jumanne saa saba mchana kwa wale wanaopenda kupiga msasa Kiswahili chao

Leave a Reply to Hyperkei Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend