MTV’s Staying Alive…Inahitaji Pongezi

Ijumaa moja nilikuwa nimetulia tu nyumbani kama kawaida nikisoma Robbo blog, kufuatilia matukio mbalimbali na kujiandaa na mechi zilizokuwa zinafuata kwenye Ligi Kuu ya Uingereza. Kwangu hiyo ni burudani tosha baada ya pilika pilika za wiki nzima kwenye maabara.

Rafiki yangu akanitumia ‘link’ ya website ambayo ilikuwa ina film ‘Shuga’, iliyotengenezwa Kenya kwa hisani ya kampeni ya MTV’s Staying Alive. Aliniambia tu, ‘Hii ni kali!’ Kama kawaida yangu nilisita kidogo; yaani niache kusoma Robbo blog halafu niangalie kitu ambacho nimekuwa nikikisikia tokea 1996 (elimu kuhusu Virusi vya Ukimwi/Ukimwi)?

Kabla ya kulala nikaamua kubofya ile ‘link’, kuangalia kilichopo huku nikiuvuta usingizi taratibu. Nilikuwa nimechoka lakini baada ya kuangalia film kwa dakika kadhaa usingizi ulitokomea. Nikaiangalia kwa makini film nzima na ujumbe nikaupata. Ni film ya zamani kidogo lakini ujumbe wake unamgusa kila kijana, hasa wale ambao wako vyuoni.

Ukiacha ujumbe uliokusudiwa kuna mambo mengine mengi ambayo yatakufumbua macho. Wale ambao wana ndoto au mipango ya kuingia kwenye fani ya utengenezaji, uongozaji wa kurekodi, uigizaji na pia utangazaji wa film nadhani watajifunza vitu viwili vitatu.

Ni film ya zamani kidogo na watu wengi labda wameshaiona, lakini nimeona sio vibaya kuianika tena na kuwapa ukumbi Vijana kuijadili.

Shuga Episode 1 from mtv staying alive on Vimeo.

Shuga Episode 2 from mtv staying alive on Vimeo.

Shuga Episode 3 from mtv staying alive on Vimeo.

Shuga Behind The Scenes from mtv staying alive on Vimeo.

Previous ArticleNext Article
Steven was born and raised in Dar es Salaam, and moved to Germany for his studies. He graduated with a BSc. in Physics (Jacobs University Bremen), and then a MSc. in Engineering Physics (Technische Universität München). Steven is currently pursuing a PhD in Physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the Netherlands. He’s thinking about starting his own business in a few years; something high-tech related. At Vijana FM, Steven discusses issues critical to youths in Tanzania, music, sport and a host of other angles. He’s also helping Vijana FM with a Swahili translation project.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend