‘Flying vaccinator’ – mbu mueneza chanjo

Picha kwa hisani ya National Geographic*

Kuna baadhi ya tafiti ambazo zinasisimua, ilihali uwezekano wake wa kuzaa matunda katika mazingira ya sasa ni mdogo. Hivi majuzi tu, wanasayansi nchini Japani wamefanikiwa kumtumia mbu kama chombo cha kusambaza chanjo dhidi ya mdudu anayesababisha Leishmaniasis. Tunajua jinsi tulivyopata chanjo utotoni; mara nyingi ilitubidi tuvumilie kudungwa sindano zenye dawa ya chanjo dhidi ya magonjwa hatari kama polio, hepatitis, kifua kikuu n.k. Katika orodha hii, yanakosekana magonjwa kadhaa (kama malaria) ambayo bado haijapatikana chanjo mahususi, kwa sababu kadhaa. Sababu kubwa ni changamoto ya kisayansi kutengeneza chanjo yenyewe, na pia gharama kubwa ya usambazaji itakayojitokeza iwapo chanjo hiyo ikipatikana.

Wajapani wamekuja na ujuzi ambao kinadharia unaweza tatua tatizo la usambazaji wa chanjo. Wameweza kumtumia mbu kusambaza dozi ya chanjo kila atakapokuwa ananyonya damu (hapa walitumia panya). Walichofanya ni kumbadili mbu maabarani ili aweze kutengeneza dawa ya chanjo dhidi ya Leishmania ndani ya gland zinazotengeneza ‘mate’ (mbu hutema ‘mate’ yake kabla ya kunyonya damu ili kuzuia damu kuganda). Wameweza kupima muongezeko wa antibodies kwenye panya waliong’atwa na hivyo kinadharia kufanikisha chanjo.

Je, si itakuwa ‘kali’ pia tukiweza kutumia mbu kusambaza chanjo dhidi ya malaria na sio mdudu mwenyewe?

Matokeo ya utafiti huu hayako kamili, kwani bado hawajapima uwezo wa chanjo hiyo kupunguza maambukizi ya ugonjwa wenyewe, ila ni tafiti pekee na ya kwanza kuweza kutumia mbu kwa namna hii. Je tutaacha kutumia sindano hapo mbeleni? Je utakubali mbu kama hawa watumiwe kusambaza chanzo za malaria hapo baadaye? Kuhusu dozi je – ukingatwa mara 1000 na mwingine mara 50? Hapa kengele ya maadili na kanuni (ethics) za sayansi inaendelea kulia.

* http://ngm.nationalgeographic.com/2007/07/malaria/finkel-text

Previous ArticleNext Article
Joji was born and grew up in Dar es Salaam, Tanzania. He graduated with a B.Sc in Biochemistry in Germany, and is now pursuing a Masters degree in Microbiology & Immunology at the Swiss Federal Institute of Technology (ETH) in Zurich, Switzerland . Joji is particularly interested in matters related to global health, and basic science research that tackles public health challenges. He is engaged in mentoring Tanzanian students in higher education issues, most notably at the Kibaha High School. In this capacity, Joji blogs with Vijana FM about scientific research and development, and how youth can gain greater access to higher learning.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend