Same old people in the Government

Steven was born and raised in Dar es Salaam, and moved to Germany for his studies. He graduated with a BSc. in Physics (Jacobs University Bremen), and then a MSc. in Engineering Physics (Technische Universität München). Steven is currently pursuing a PhD in Physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the Netherlands. He’s thinking about starting his own business in a few years; something high-tech related. At Vijana FM, Steven discusses issues critical to youths in Tanzania, music, sport and a host of other angles. He’s also helping Vijana FM with a Swahili translation project.

This post has 5 Comments

5
  1. I saw the ad, interesting. I am not surprised that this add is banned, its election year, and this add doesn’t help Hon Kikwete and CCM’s presidential campaign. Who wants to hear the truth, who wants the people to be inspired to think and start asking question, of course thats the last thing they would want to happen. Haven’t you seen how they managed to avoid the presidential debate, with lame excuses. Kikwete is too busy, really?, so is everyone else who is campaigning.

    The thing is this, they know there are a lot of questions that they dont have answers for.

    Mimi mpaka sasa sielewi ni kitu gani kimewatisha wakubwa na hili tangazo, kwani ahlisemi kitu chochote kipya ambacho hatukijui.

    Video za hawa kuweniserious ni nzuri sana, kwani hili suala la wazee walele kila uchaguzi limezidi. Lakini, pamoja tunaweza lalamika, swali ni hili, je sisi vijana tunafanya nini kuhakikisha hali hii inabadilika? Kama alivyosema Bill, hakuna watu mbadala, hivyo wale wale wanaendelea kugombea miaka nenda rusi.

    Lakini nimeona mwaka huu kuna wazee fulani fulani wameangushwa, nadhani hiyo ni ishara njema.

  2. Mzee, uchaguzi huu umekuja na mbwembwe za kila aina. Yaani mi’ nimeshaanza kuusubiri wa 2015. Kama ingekuwa ligi kuu ya kandanda, nadhani haya tunayoona sasa hivi ni kama kipindi cha usajili wa wachezaji tu!

    Ila mambo sio rahisi kihivyo. Ingawa kuna mwamko fulani sasa hivi, bado vijana wengi sana hawajui “kinachoendelea.” Wanafuatilia siasa juu juu tu. Sasa kijana ambaye hafuatilii na kusoma kwa undani ilani za vyama, unadhani baadae atakuja kuwa kiongozi mzuri?

    Ukiacha hayo, mpaka pale vijana watakapogundua kuwa WANAWEZA basi tutaanza kuona mabadiliko. Lakini hii ya kelele zisizokuwa na mpangilio haitatufikisha mbali. Kinachohitajika ni kuwa na dhamira na mpangilio wa utendaji. Kwasababu vikwazo na changamoto ni nyingi mno, na wachache wanaoingia kichwa kichwa ndio wanakuja kukata tamaa. Lakini kukiwa na umoja fulani hivi mambo yatakuwa sio magumu sana.

    Vijana wa Tanzania inabidi wasome na kuelewa mabadiliko ya nchi kama Afrika Kusini, Burkina Faso na hata nchi za magharibi ili kujifunza mawili matatu.

    Ninachojaribu kusema ni hiki: Mabadiliko yaliletwa baada ya vijana KUJIPANGA na kujenga dhamira isiyotetereka. Sisemi watu wapindue nchi. LA HASHA! Naongelea jinsi watu walivyojipanga ili kutovipa vitu fulani (uwizi wa kura, vitisho, rushwa, hongo, ubadhirifu n.k.) mwanya wa kutokea; kwa kuwa hivi ndivyo hutumiwa na status quo ili kunyamazisha vijana.

    Watu mbadala wapo nadhani. Ila, kwanini waache wanayoyafanya ili kupigana vita ambayo wanajua — kwa uhakika — kuwa watashindwa? Ndio maana naelewa watu wenye misimamo kama ya Bill…

    Kwa kumalizia tu, napenda kusisitiza kuwa kuna tofauti kati ya “kulalamika” na “kukosoa.”

  3. Nimeangalia hiyo video na nashawishika kuamini kuwa pengine vijana wa Kenya wana uelewo mkubwa zaidi kuhusu politics za Kenya kuliko sehemu kubwa ya vijana wa kitanzania.Inaweza kuwa ni ukweli unaouma lakini unabaki kuwa ukweli.

    The dude in the video is some celebrity kijana ambaye ana influence katika jamii.Nimependa jinsi ambayo anazungumzia issues napata shida kuamini kuwa tuna wasanii wengi hapa Tanzania wanaoweza kujitokeza na kuongea bila woga juu ya concerns zako katika siasa.

    Wasanii wetu ni watu wanaofikiria matumbo tu na si kwasababu wana-support chama tawala tu lakini hapajakuwa na involvement ya maana ya wasanii wa kada mbalimbali kujiingiza katika kupigania haki za wanyonge.

    Nafikiri ni wakati mzuri sasa wa kujifunza toka kwa wenzetu!

  4. EP, wakati kina Ismail Jussa wakijaribu kufundisha umma kasoro zilizopo kwenye katiba, watu wanaziba masikio. Ngoja tu hii EAC ichanganye; sitashangaa wageni wakinukuu na kukosoa vifungu vya katiba yetu. Hapo ndio laaaabda vijana wa Tanzania wataanza kufuatilia siasa kwa makini.

    Siongelei hizi siasa za ushabiki na kuandika “status” mpya kila saa (facebook na kuvaa t-shirts). Naongelea ufuatiliaji (na uchambuzi) wa ilani za vyama, katiba na utendaji wa Serikali. Ulizia mitaani watu wangapi wanaelewa mapungufu ya Katiba ya Muungano (wakati tuna katiba mbili tu: ya Zanzibar na ya Muungano).

    Kuna mtu alituma swali kwa Michuzi wiki chache zilizopita.. alikuwa anataka kujua itakuwa vipi kama kambi ya upinzani Tanzania Bara ikipata viti vingi Bungeni.

    Wazanzibari katiba yao inaruhusu kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Sidhani kama ya Muungano inaongelea na kuweka hilo jambo wazi (nisahihisheni kama nimekosea).

    Wachangiaji wakamjibu: “Mbona ASP na TANU vilikuwa vyama tofauti lakini vikaweza kuunda Serikali ya Muungano!?”

    EP, ukitaka kuona video nyingine za Kuweni Serious, search “Kuweni Serious” hapo juu…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend