Elimu kwa njia ya puku

Vijana wa mwaka ‘arobaini na saba’ walikuwa wakitumia nafasi ya kujifunza stadi mbalimbali kupitia mpango wa Elimu kwa Njia ya Posta. Karne hii, kwa walio na access ya internet tungependa kuhimiza matumizi ya Elimu kwa Njia ya Puku. Katika miaka inayokuja Vijana FM inajipanga kuwa mwezeshaji wa aina hii ya elimu kwa ajili ya mazingira na mahitaji ya Afrika Mashariki. Ila kwa sasa, mtandaoni kuna rasilimali tele ambazo vijana tungependa wazitumie kuongeza wigo wao wa kielimu na maarifa. Rasilimali hizi zinazopatikana kwa njia ya video, na ni bure, zinatolewa na taasisi na vyuo vikuu mashuhuri duniani kwa ajili ya masomo binafsi ya wanafunzi.

Tutaendelea kuipigia filimbi KHAN Academy kwa kuwa tovuti hii ina ‘utirio’ ulioshiba katika kila mada utakayofikiria. Ukitaka kupata mandhari ya kidarasa, basi tembelea tovuti ya Chuo Kikuu cha California — Berkeley na kuperuzi mihadhara mbalimbali zinazotolewa na wahadhiri waliobebea katika nyanja zao — kwa mfano, kuanzia elimu ya Astronomy, Afya ya Jamii, Sheria za Hatimiliki mpaka Historia ya China!  Zote utakumbana nazo humo. Bonyeza nembo zifuatazo kwa zaidi.

Tafadhali tembelea kurasa yetu ya ‘Resources‘ hapo juu ili kufahamu tovuti nyingine kadhaa za aina hii.

Tunapiga parapanda hii sio tu kwa wale walio vyuoni, bali pia kwa yeyote ambaye angependa kujiendeleza kimaarifa katika nyanja mbalimbali.

Previous ArticleNext Article
Joji was born and grew up in Dar es Salaam, Tanzania. He graduated with a B.Sc in Biochemistry in Germany, and is now pursuing a Masters degree in Microbiology & Immunology at the Swiss Federal Institute of Technology (ETH) in Zurich, Switzerland . Joji is particularly interested in matters related to global health, and basic science research that tackles public health challenges. He is engaged in mentoring Tanzanian students in higher education issues, most notably at the Kibaha High School. In this capacity, Joji blogs with Vijana FM about scientific research and development, and how youth can gain greater access to higher learning.

This post has 2 Comments

2

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend