Antivirus Mixtape iko jikoni…

Msanii mkongwe Sugu au kama alivyokuwa akifahamika enzi zile kama Mr II anakuja na album itakayoitwa antivurus. Mixtape hii itakayoshirikisha wasanii wengi wa bongo flava, inakuja kwa dhumuni la kupigania sanaa hii na kupigania haki ya badhii ya wasanii wa sanaa hii ya bongo flava na bongo hip hop.

Hivi karibuni kumekuwa na mijadala kadhaa kuhusu mwelekeo wa sanaa ya bongo flava, lakini kidogo kimekuwa kikifanyika kuitetea ipasavyo. Katika makala ya penye kufuka moshi niliweza kujadili uhasama unaoanza kujengeka kati ya wasanii wapya na wale wakongwe. Wasanii wakongwe wamekuwa wakiwalaumu wasanii chipukizi kuwa wanachangia katika kuudhofisha mziki huu wa bongo flava. Nadhani kila mtu analake la kusema juu ya malumbano haya, kutegemeana na upande unaoshabikia.

Shauku yangu na hii mixtape ya antivirus ya Sugu ni kuwa itasaidia kuweka hili tatizo bayana kwa kuwataja wahujumu wakuu wa sanaa hii. Nadhani muda umefika kwa baadhi ya wasanii kuweka msimamo na kusimama pamoja kutetea mziki huu. Tuombe harakati hizi ziweza kuzaa matunda, kwani wengi wanaamini mziki huu umepoteza dira kwa kiasi fulani, sasa sijui kama wewe unakubaliana au kupingana na hoja hii.

Habari hii kwa hisani ya bongo5.com

Previous ArticleNext Article
Bahati was born and raised in Tanzania, and then moved to California to pursue his college education. He graduated in 2008 with a Bachelor’s Degree in Political Science and a minor in Sociology. Bahati expects to be doing his Masters in African Studies in the near future. He is currently working on starting a t-shirt business and a possible publication of some of his writings. One thing that Bahati cannot live without is music, specifically Hip Hop & Bongoflava which he argues are both the voice of the youth today, and is excited to look into how Bongoflava can be a source of further entrepreneurship among the youth in Tanzania. Bahati believes that Bongoflava can help to reduce poverty in Tanzania, as can a more collective effort among key players.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend