Tovuti ya Wahapahapa Na Sanaa..

Leo hii sanaa bado haijapewa heshima na kipaumbele kama inavyotakiwa, pamoja na sanaa kuwa kioo cha jamii. Tovuti na blog zimeanza kumea kama uyoga, lakini chache zimekuwa zikitetea nafasi ya sanaa katika jamii na haki na umuhimu wa wasanii ndani ya jamii.

Wahapahapa ni moja ya tovuti ninazoweza kusema zimejikita katika sanaa, siyo kuishia kuzungumzia sanaa tu. Kitu kilichonifurahisha na tovuti ya wahapahapa, ni kuwa wameweka michezo ya kuigiza ya redio katika tovuti yao. Hii inawapa fursa hata walio mbali kufaidi sanaa hii kongwe iliyopewa kisogo kutokana na ukuaji wa utandawazi. Nadhani kizazi cha enzi zile tunaweza kukumbuka ile michezo ya akina marehemu Pwagu na Pwaguzi katika redio ya Taifa, RTD.

Tembelea tovuti hii ya Wahapahapa na sikiliza michezo hiyo ya kuigiza na pia kujisomea mambo mengi mengineo ya kuelimisha kupitia sanaa.

Previous ArticleNext Article
Bahati was born and raised in Tanzania, and then moved to California to pursue his college education. He graduated in 2008 with a Bachelor’s Degree in Political Science and a minor in Sociology. Bahati expects to be doing his Masters in African Studies in the near future. He is currently working on starting a t-shirt business and a possible publication of some of his writings. One thing that Bahati cannot live without is music, specifically Hip Hop & Bongoflava which he argues are both the voice of the youth today, and is excited to look into how Bongoflava can be a source of further entrepreneurship among the youth in Tanzania. Bahati believes that Bongoflava can help to reduce poverty in Tanzania, as can a more collective effort among key players.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend