Kongamano la Vijana Kilimanjaro

Vijana wanachama wa YUNA (Youth Of United Nations Association) mkoani Kilimanjaro wanategemea kufanikisha kongamano la vijana litakalohusu ushiriki wa vijana katika uchaguzi mkuu Oktoba 2010 na mapambano ya vijana dhidi ya rushwa wakati wa uchaguzi.

Kongamano hili lenye manufaa kwa jamii nzima ya Watanzania linatarajiwa kufanyika tarehe 21 Agusti, 2010 katika ukumbi wa Kilimanjaro Cranes uliopo Moshi Mjini.

Lengo la kongamano hili ni kuwahamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za Uchaguzi Mkuu kwa kuwa vijana ndio nguzo kuu ya Taifa!

Vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika:

Washiriki wa kongamano hili:

  • Wanachama wa YUNA wanafunzi (sekondari na wanavyuo)
  • Wanachama wa YUNA wasio wanafunzi (wahitimu wa kidato cha sita na vyuo)
  • Vijana wasio wanachama wa YUNA

Washiriki wasio wachangiaji:

  • Wanasiasa
  • Waandishi wa habari
  • Viongozi wa Serikali
  • Walezi wa YUNA na asasi nyingine za kiraia

Kongamano litaendeshwa kwa lugha ya Kiswahili na litakuwa katika muundo wa mdahalo; ambapo kutakuwa na washiriki watakaopewa fursa ya kutoa maoni yao, kujenga hoja, kupinga hoja na kufanya marekebisho ya baadhi ya hoja zitakazotolewa.

Shukrani kwa Japhet Joseph kwa kutuletea ujumbe huu. Na timu ya Vijana FM inawatakia kila la kheri kwenye kongamano!

Previous ArticleNext Article
Steven was born and raised in Dar es Salaam, and moved to Germany for his studies. He graduated with a BSc. in Physics (Jacobs University Bremen), and then a MSc. in Engineering Physics (Technische Universität München). Steven is currently pursuing a PhD in Physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the Netherlands. He’s thinking about starting his own business in a few years; something high-tech related. At Vijana FM, Steven discusses issues critical to youths in Tanzania, music, sport and a host of other angles. He’s also helping Vijana FM with a Swahili translation project.

This post has 1 Comment

1

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend